Wednesday, December 12, 2012

MKUTANO WA INJILI ULIOENDESHWA NA PR MAPIMA

KANISA LA UKONGA SDA 



TUWAPIME     MANABII    /    MITUME    WA    SASA
          NA MIUJIZA YAO     
    KATIKA MIZANI YA HAKI

____________________________________________________________________________________
§  UTANGULIZI

§  KWANINI KUWAPIMA WANAODAI NI MANABII?

§  MTU ANAKUWAJE NABII?

§  SIFA 5 ZA NABII, JE! WANAODAI NI MANABII TANZANIA WANAZO SIFA HIZO?

§  JE!  MIUJIZA  NI  KIPAUMBELE AU KIINI CHA  KAZI YA  UTUMISHI  YA  NABII?

§  NA JE! MIUJIZA YA MANABII HAO KUANGUSHA WATU CHINI NI YA KIBIBLIA?

§  ONYO JUU YA WATUMISHI WA UONGO KWA KIZAZI CHA NYAKATI ZA MWISHO.

IMETAFITIWA NA KUANDALIWA NA MCHUNGAJI-   MHADHIR: DOMINIC MAPIMA
Email: dominicmapima@yahoo.com/ Mobile 0715 527143


Utangulizi
Ninachukua fursa hii kwanza kukusalimu mpendwa msomaji wa makala hii nyeti ya kuwachunguza Manabii na Mitume wanaoibuka katika Ulimwengu lakini hususani katika nchi yetu ya Tanzania, Amani ya Bwana Yesu iwe juu yako!
Baada ya salaamu nipende kumshukuru sana Mungu Baba wa mbinguni kwa kukuweka salama katika maisha yako hadi saa unapoisoma makala hii.
Mimi binafsi ninamshukuru Mungu pia kwanza kwa uzima, lakini pili kwa kutimiza shauku yangu ya kiutafiti na uandishi wa makala hii ili kufungua macho watu wa Mungu wanaobaki kuchanganyikiwa au kutekwa na hali hii ya sintofahamu ya kuibuka kwa wimbi kubwa la watu wanaodai kuwa ni watumishi, mitume na manabii na kufanya maajabu mbalimbali na miujiza huku wakidai haki ya kuaminiwa na kukubalika kama sehemu ya mitume na manabii wa kweli wa Mungu wa kibiblia.
Kabla ya kuandika makala hii nilisumbuka kwa muda mrefu ndani ya moyo wangu kuona hali hii ikishika kasi katika nchi yetu ya Tanzania kwa kiwango cha juu na zaidi kukutana na watu mbalimbali walioumizwa na vuguvugu hili la kuibuka kwa watu hao wanaodai kuwa ni watumishi tena katika daraja hilo la mitume au manabii.
Msukumo wa kuandika makala hii kutokana na shuhuda za kitapeli
ü  Nikiwa katika mahubiri mnamo mwezi wa 9/2011 katika eneo la kidatu, dada mmoja alikuja kwenye mkutano akiwa na bahasha yenye pesa’ baada ya kuhojiana na wahudumu wa kwaya alijieleza kuwa ameleta bahasha hiyo baada ya kuhudhuria mkutano Fulani ambapo mhubiri alijitambulisha kama mtume na Nabii’_mhubiri huyo aliwataka wenyeshida mbalimbali waende wakaombewe ambapo dada huyo pia alijitoa kwenda kuombewa’ baada ya maombi hayo, mtumishi (mtume) huyo alitangaza kuwa wote walioombewa wanapaswa kupeleka sadaka ya Tsh 3000/= kama shukrani ili Mungu aridhie maombi yao Na kama wasingefanya hivyo wangeweza kufa,hivyo dada huyo kwa hali duni sana ya maisha aliyokuwa nayo alichelewesha kupelekwa fedha hiyo’ na kwakuwa mkutano ulishakuwa umefungwa basi aliamua kuleta fedha hiyo mkutanoni kwetu kwa kudhani kuwa sisi tuko pamoja na mtumishi huyo. Ili kuepuka hukumu hiyo.
Mpendwa msomaji wangu, tendo la kukutana na tukio hili lilizidi kuamsha msukumo niliokuwanao moyoni mwangu wa kuandika makala hii maalumu ya Kibiblia ili kusaidia maelefu ya watu waliofungwa kihisia na kiimani hivyo kuzama katika kuwaamini watumishi hao wa uongo.
Msukumo wa kuandika makala hii kutokana na kuhushwa hadhi cheo cha Unabii, Utume

Msukumo wa kuandika makala hii kutokana na Wimbi la maombezi na Miujiza ya ajabu




TUCHUNGUZE IMANI
                                        Pr  Dominic  Mapima.
                    Somo la ‘8’ Mahubiri ya hadhara – Ukonga SDA.
NEEMA NA  SHERIA  KATIKA JUKWAA LA UTAKASO
UTANGULIZI
PAMOJA NA KUJIFUNZA KWA KINA JUU YA KIOO CHA MSAFIRI WA IMANI YAANI SHERIA AU AMRI KUMI ZA MUNGU NA UMUHIMU WAKE KWA WAFUASI WA IMANI, BADO LIKO HITAJI JINGINE LA KUFANYA MAPITIO YA MADA HII ILI KUWEKA BAYANA UKWELI JUU YA DHANA MBALIMBALI ZISIZO SAHIHI ZINAZOIBUKA JUU YA SHERIA ZA MUNGU KWA KILE KINACHODAIWA KUWA SHERIA HIZO ZA MUNGU ZILIKOMA KUFUATIA TENDO LA KIFO CHA YESU MSALABANI, KIFO AMBACHO KILIFUNUA KITU KINACHOITWA ‘NEEMA’ (MSAMAHA WA BURE).NA HIVYO KUDAIWA KWAMBA NEEMA HIYO INAONDOA AU KUKOMESHA SHERIA’ (AMRI KUMI).
KATIKA KUWEKA MSISITIZO WA MADAI HAYO, WALIMU NA WAHUBIRI HAO WALIOIBUA FARSAFA HIYO WAMEKUWA WAKITUMIA MAFUNGU KADHAA YA MAANDIKO YA BIBLIA KWA KILE KINACHODHANIWA KUWA MAANDIKO HAYO YANAUNGA MKONO FARSAFA HIYO YENYE UTATA
Efeso 2;8 Kwa  maana  mmeokolewa  kwa neema, kwanjia ya imani, ambayo
                hiyo haikutokana na nafsi zenu,ni kipawa cha Mungu. (9) wala si kwa
              matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
Galatia 3:11Ni dhahiri ya  kwamba hakuna  mtu  ahesabiwaye  haki mbele za
               Mungu katika sheria, kwasababu  mwenye haki ataishi kwa imani.
Hayo ni baadhi ya mafungu ya Biblia yanayotumiwa kukaza hoja hiyo juu ya kile kinachodaiwa kuwa mafungu hayo yanatoa madai ya  kutokuwepo kwa umuhimu tena wa sheria za Mungu kutokana na mafunuo ya neema ya Kristo kwa kifo cha masalaba na hivyo wenye haki wa Mungu wataishi kwa imani na hakuna haja tena ya sheria au amri za Mungu katika maisha ya muumini.
HIVYO BASI’ KUPITIA SOMO HILI TUTAANGALIA KWA UMAKINI ILI KUPATA UELEWA WA MSINGI JUU YA MAHUSIANO YA NEEMA NA SHERIA KATIKA JUKWAA LA UTAKASO, LAKINI PIA KUONA KAMA MADAI HAYO NI YAKWELI AU NI TAFSIRI TU INAYOTOLEWA KAMA MATOKEO YA KUTOYASOMA MAANDIKO KWA UMAKINI.
KOSA LA UMAKINI KATIKA USOMAJI WA BIBLIA
Kile kinachoonekana kuwa ni tatizo la waalimu wengi wanaeneza farsafa hii isiyo sahihi, ni uelewa husiyo wa kina juu ya mfumo mzima wa mafunuo ya “sheria” katika maandiko ya Biblia.
Ni kosa kubwa sana katika taaluma ya usomaji wa Biblia kutojua muundo wa mafunuo ya sheria hivyo kutoweka tofauti unapojadili au kusema lolote juu ya mafunuo hayo ya sheria, na pengine niseme kuwa hata changamoto hii ya madai ya kukomeshwa sheria (amri kumi) imezaliwa kutokana na makosa hayo ya wale wanaofundisha kutokuwa na kina cha uelewa juu ya mifumo ya sheria katika Bilblia na hivyo kuelewa kazi za sheria katika aina zake na uhusiano wake na neema ya Kristo kwa kifo cha masalaba.
Walimu wengi leo wanasoma Bibli kwa kubahatisha/ tumekuwa kama vipofu.
Mfano;
Eg; kulikuwa na vipofu wawili ambao walitamani kufahamu umbile la tembo,bahati njema Serikali yao iliandaa fursa maalumu kwa walemavu kwenda kufanya utalii wa kufahamu wanyama hao,wakiwa katika banda maalumu alipohifadhiwa tembo aliyetulizwa kwa madawa maalumu, vipofu hawa waliingizwa kwa zamu ili kumgusa tembo huyo, ili kufahamu umbile lake’ kipofu wa kwanza-alimgusa kwa hofu kubwa kwenye mkonga akishusha na kupandisha mkono’ na ghafla aliruka kwa shangwe huku akidai kuwa amegundua kwamba tembo anafanana na nyoka!!!’/ kipofu wapili naye –alishika eneo la sikio la tembo na kupitisha kiganja mithili ya mtu anayesuuza chombo ndipo naye ghafla alionekana kurukaruka huku akidai kuwa tembo anafanana na sahani ya kulia ugali!!!
Kimsingi vipofu hawa wote walipata nafasi ya kumchunguza tembo, lakini kile kinachoonekana kuwa ni kosa kwao ni aina ya uchunguzi na viwango vya uchunguzi wao huo viliwaletea majibu yasiyoendana na ukweli halisi juu ya umbile hasa la mnyama huyo’ tembo. Kosa hili ndilo linalotendwa katika ulimwengu wa kidini leo na hivyo kupelekea kuibuka kwa farsafa mbalimbali zisizo za haki hivyo kuwachanganya wafuasi waaminifu wa dini.
KUWEKA  TOFAUTI  YA SHERIA  KATIKA  BIBLIA.
Kanuni ya kwanza muhimu katika ufumbuzi wa changamoto hii ni kuchunguza mfumo wa sheria katika Biblia, inaweza kuwa swala rahisi kuelewa mafungu mbalimbali ya Biblia yanayozungumzia kukoma kwa sheria nk, ikiwa tu tutakuwa na uelewa sahihi juu ya muundo wa mafunuo ya sheria katika Biblia.
Mungu alipofunua sheria zake aliweka tofauti, hivyo pamoja na kuwepo kwa makundi mengi ya sheria tunaweza kufanya migawanyo ya ufupi ya sheria kama ifuatavyo:-
Moral Laws – Sheria adilifu’
Social Laws – Sheria za kijamii’
Ceremonial Laws – Sheria za sherehe za makutaniko na kafara’
Huo ni mgawanyo mdogo wa mafunuo ya sheria katika maandiko ya Biblia, hivyo utagundua kwamba kwa kadri ya Biblia unapozungumzia sheria unaongelea uwanja mpana sana wa kiuchambuzi.
Namna Biblia inavyoweka tofauti ya sheria
Biblia inagawanya sheria hizi katika makundi makuu mawili ya msingi.
Moral Laws – Sheria adilifu, “amri kumi za Mungu” – hili ni kundi muhimu sana la la sheria (amri) za Mungu, Biblia inaweka tofauti ya sheria hizi na zile nyingine za kijamii yaani Social Laws na Ceremonial Laws, na kwajumla kundi hili la pili hutajwa kama “sheria za Musa au Sheria za maagizo”, hivyo pia maandiko ya Biblia yameweka kanuni bora ya jinsi ya kuweka tofauti ya sheria hizi kama ifuatavyo:-
1.      Tofauti ya kwanza.
§  Amri kumi ‘Moral Laws’ – Ziliandikwa na Mungu mwenyewe  Kutoka 31:18.
§  Sheria za Musa/Maagizo’- Ziliandikwa na  Musa 2nyakati 35:12.

2.      Tofauti ya pili.
§  Amri kumi’ Moral Laws’- Zilihifadhiwa katika sanduku la agano. Kumb 10:5
§  Sheria za Musa/Maagizo- Ziliwekwa kando ya sanduku.      Kumb 31:24 -26
Kwa msingi huu wa mgawanyo wa Sheria ,unaweza kugundua kuwa kabla mtu hajajenga hoja yeyote juu ya sheria  lazima ajue aina  ya  sheria anazozikusudia.
Na kutokana na kutozingatia hilo baadhi ya viongozi na wahubiri wa dini wamesikika wakitoa tafsiri na maelezo ya jumla yanayogusa mustakabali wa sheria hizi pasina kuweka tofauti yeyote tendo liliozua tafsiri batili kuwa kifo cha Yesu kililenga kukomesha aina zote hizo za sheria, na hivyo kwasasa sheria za  Mungu hazina kazi tena katika maisha ya waumini kwa kuwa tunaishi kipindi cha neema.
JE’ NI AINA GANI YA SHERIA INAYOKOMESHWA NA NEEMA?
Kwa kujifunza mgawanyo huo wa sheria katika Biblia, ndipo unaweza kujiuliza swala hilo la busara kuwa  je’ mauti ya Yesu au Neema ya msalaba inakomesha aina gani ya sheria? ni zile adilifu (amri kumi – moral laws) au ni zile za Maagizo? (Sheria za Musa/ceremonial laws – social laws)?.
Neema haikukomesha amri kumi ( Moral Laws) bali amri (sheria) za maagizo.
Tunapozungumzia neema maana yake tunazungumzia mauti ya Yesu msalabani iliyoleta msamaha wa bure husiyotokana na kustahili kwetu,msingi au kusudi la mauti ya Yesu ilikuwa ni kutimiza madai ya torati juu ya utakaso wa dhambi na ukombozi wa nafsi..
Ebrania 9:22 Na katika Torati vitu vyote husafishwa kwa damu na pasipo
                    Kumwaga damu hakuna ondoleo.
Madai hayo ya torati hapo awali yalitimizwa kwa njia ya kuchinja wanyama maalumu kama tendo la kafara au fidia ya uovu na makosa ya mwanadamu kwa Mungu ambapo maelekezo hayo ya uchinjaji wa wanyama kama ishara au kielelezo cha neema iliyokusudiwa kuja ndiyo yaliyotambuliwa kama sheria za makafara’ Ceremonial Laws’, kwa msingi huo Yesu alipokufa msalabani alichukua nafasi ya wanyama hao nay eye kuwa ndiye kafara halisi ya dhambi zetu, na hivyo kwa hali hiyo ile sheria ya uchinjaji wa wanyama inakoma.
Kwa muktaza huo inakuwa ni sahihi kusema kuwa neema ya Yesu imekomesha sheria hiyo kwamaana sasa watu hawana haja tena ya kuchinja wanyama kama tendo ya kafara ya dhambi kadri ilivyoamriwa katika sheria ile ya makafara. Rejea:- lawi 22:19-21/  lawi 23;26.
Lakini kile kinachoonekana ni kuchanganya mawazo ya Kibiblia, ni pale baadhi ya wahubiri wanaposikika wakihubiri kwa ujasiri kuwa mauti hiyo ya Yesu ililenga kukomesha aina zote za sheria, na hivyo sasa tunaishi chini ya neema hivyo hakuna haja tena ya amri , sheria za Mungu wakimaanisha kuwa hata amri zile kumi (adilifu zilizoandikwa na Mungu mwenyewe) zimekoma, na hakuna haja ya kuwekea maanani amri hizo’ fundisho hilo ni la hatari sana.
AMRI KUMI NI ZA MILELE, ZINAFANYAKAZI NA NEEMA.
Mbali na sheria hizo nyingine za maagizo zinazokomeshwa na mauti ya Yesu msalabani, amri kumi za Mungu zilizoandikwa kwenye mbao za mawe zinadumu milele, kimsingi amri zile kumi ndiyo tabia halisi ya Mungu anayohitaji sisi wanadamu tuiakisi ili tudumu kuitwa wana na binti zake.
Mambo yanoyothibitisha kuwa amri hizo ni za kudumu.
-          Ziliandikwa kwa kidole cha Mungu mwenyewe “Mhubiri 3:14.
-          Ziliandikwa kwenye mbao za mawe; ni ishara ya kudumu. “Kumb 9:9-11
-          Biblia inazitaja ni za milele  Zaburi
Sababu ya msingi ya kudumu kwa amri kumi:-
-          Ndiyo kauli mbiu ya Mungu juu ya vile mwanadamu anavyopaswa kuenenda na hivyo kuakisi tabia yake. “Zaburi 40:8 kuyafanya mapenzi yako.... ndiyo furaha yangu,.... sheria yako imo moyoni mwangu
-          Ndicho kipimo cha haki na ubatili, kuelewa imani sahihi, watumishi wa kweli na wauongo wanapimwa kupitia mwenendo wao na utii wa amri hizi.
Isaya 8:20 Na waende kwa sheria na ushuhuda kama hawaendi sawasawa.....
-          Ndiyo msingi wa kazi ya kanisa duniani, kwakuwa kazi ya kanisa ni kutangaza mapenzi ya Mungu ambayo kimsingi yanafunuliwa katika amri zake, hivyo kanisa lipo ili kutangaza mapenzi ya Mungu(amri /sheria zake)
Yohana 14:15 mkinipenda mtazishika amri zangu.
-          Amri za Mungu zinadumu pia kwasababu bado huduma ya upatanisho wa dhambi inaendelea katika hekalu la mbinguni na amri za Mungu ni shahidi wa matendo kama ilivyokuwa katika hekalu la dunia.
Ufunuo 11:19 Hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa..na sanduku la agano lake likaonekana mbinguni....
Kwa uchambuzi huo wa maandiko unaweza kugundua ndugu msomaji kuwa amri kumi za Mungu ndiyo uti wa mgongo wa kusudi zima za Mungu kushughulika na wanadamu, na jambo lenye uzito zaidi ni kuwa neema ya Yesu msalabani ili ifanyekazi lazima kuwepo na sheria/ amri za Mungu.
Kazi ya Neema na Sheria/ je Neema inaondoa sheria?.
Neema ni nini?  Ni msamaha wa bure unaotolewa na Mungu kwa huruma
                                zake kwa mwanadamu mdhambi pamoja na kutostahili
                                kwake.
Sheria ni nini?   -    Ni mafunuo ya maelekezo au maagizo ya tabia na usafi wa
                                Kiroho ns kimwenendo anaopaswa kuwa nao mwanadamu ili
                                kuunganishwa kitabia na Mungu.
Uhusiano wa Neema na Sheria’
Kazi ya Neema:
Tito 2:11 Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa;
             (11)nayo yatufundisha kukataa ubaya na  tamaa za kidunia; tupate
             kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa.
Andiko hili ndilo linalofunua kazi ya Neema’ na kama umefatilia vizuri fungu hilo utagundua kuwa kwajumla kazi ya Neema ni kutoa uwezo wa ushindi kwa mwanadamu dhidi ya matendo ya dhambi.
Kwakuwa kazi ya Neema ni kumwezesha mwanadamu kuishinda dhambi basi utagundua kuwa ili Neema ifikie kusudi hilo lazima isaidiane na sheria kutokana na kazi ya sheria inayoelezwa kupitia kitabu cha Warumi, hebu tusome:-
Warumi 7:7 Tusemeje basi? Torati ni dhambi? Hasha! Walakini singalitambua
                  dhambi ila kwa sheria; kwakuwa singalijua kutamani, kama Torati
                  isingalisema, usitamani.
Hivyo dhambi hujulikana kwa njia ya sheria, na tutakubaliana ndugu msomaji kuwa haiwezekani kupambana au kuishinda dhambi ikiwa hujui kuwa hiyo ni dhambi’;“Hata wachezaji wa mpira hawaendi katika shindano pasipo kujua uwezo na mbinu za timu pinzani’ huweza hata kutuma watu kupeleleza wenzao’.
Kwahiyo kimsingi, Neema na Sheria hufanya kazi pamoja, yaani Sheria hufunua dhambi na Neema hutoa uwezo kwa mdhambi kuishinda.
Kwamaana hiyo’ si jambo sahihi kutafsiri kuwa Neema imekuja kuondoa sheria za Mungu ( Amri kumi)., na kwadri ambavyo Neema na sheria hufanyakazi kwa pamoja, kusema kuwa Neema imeondoa sheria kunamuingiza mtu anayedai hivyo kwenye kosa pana la kufuta kabisa uwepo wa kanisa, kwasababu:-
“Bila sheria HAKUNA DHAMBI/ kama hakuna dhambi basi HAKUNA HAJA ya NEEMA/ na kama hakuna neema basi HAKUNA MSALABA/ kama hakuna msalaba basi hakuna WOKOVU/ kama hakuna wokovu basi HAKUNA KRISTO MWOKOZI/ kama hakuna Kristo basi hakuna UKRISTO/ kama hakuna ukristo basi HAKUNA KANISA
Mfano
Utendaji wa Sheria na Neema.
Eg; Neema na Sheria ni sawa na Trafic na Garage/ ikiwa umepata ajali kwa gari yako kugongwa na gari nyingine, huwa anaitwa Trafiki, kazi ya Trafiki ni kuonyesha kosa ni la nani kwa mujibu wa sheria, hivyo Trafiki ni Sheria’na baada ya funua mkosaji si jukumu lake kuombwa kutibu madhara ya ajali kwa kunyoosha gar ink, jukumu hilo hufanywa na gereji’ hivyo gereji ndiyo neema. Hivyo huwezi kusema kwasababu tuna geriji za kunyoosha magari basi hakuna haja ya sheria za barabarani.
Mfano
Sheria zinakuonyesha kosa nawe unatafuta Neema.
Eg; kibaka mmoja alipora mtu simu, watu walimkimbiza wakiwa na silaha kali, hatimaye wakafika mahali ambapo kulikuwa na njia 2’ moja ni ndefu sana ambayo kama angepita hiyo wangeweza kumpata, lakini njia ya pili ilikuwa ikielekea kituo cha polisi, kwa kadri ya hatari hiyo alitambua kuwa kwa ukosaji huo ni bora ajisalimishe polisi ambapo labda angepata rehema na kuepuka mauti’...sheria inakufanya utambue kosa, na kosa hilo litakuongoza kuitafuta neema kwa kuwa utajiona kuwa ni mhitaji.
Hatari kwa wanaokataa sheria’
Kile kinachoonekana kuwa ni hatari kwa wale wanaopinga mafunuo ya sheria ni hisia za kujiona wenye haki.
Kumbuka neema inahitaji mtu anayejiona kuwa ni mdhambi anapojipima mbele za MUNGU ili apate rehema, visa na mafungu yafuatayo vinaweka wazi:.
1yohana 1:8-10 tukisema kwamba hatuna dhambi twajidanganya
Mathayo             Sadukayo  na  farisayo  walikwenda  kuomba,  Farisayo
                            alijihesabia haki, lakini Sadukayo alisema yeye ni mwenye
                            dhambi..huyu ndiye aliyekubaliwa toba yake....

MAFUNGU YANAYONESHA KUDUMU KWA AMRI ZA MUNGU KATIKA AGANO JIPYA
Katika kipindi cha injili bado Mungu aliendelea kusisitiza juu ya ya umuhimu wa kutunza amri na sheria zake, kupitia kwa kinywa cha Yesu mwenyewe na mitume wake’
Unaweza kusoma mafungu yafuatayo kuona jambo hili la msingi’
Mathayo 19:17 ..ukitaka kuingia ufalme wa Mungu shika amri..
Luka 1:5 ....Zakaria na Elizabeti walishika amri zote za Bwana..
Rumi 8:3 ...maagizo ya Torati yatimizwe ndani yenu...
1wakoritho 9:20 ... Ni mwenye sheria mbele za Kristo..

Watu wa kihistoria waliopenda amri za Mungu
Msafiri mvumbuzi  Sir HENRY MORTON  STANLEY – alimsomea Chief wa Afrika amri kumi/ naye aliomba watu wake wafundishwe amri hizo, alisema endapo watu wake wakijua amri hizo atakuwa mfalme pekee mwenye taifa lenye watu wenye upendo wa kweli’.
Mwanafarsafa Emmanuel Kant, aliwahi kusema; hakuna sehemu tukufu katika maandiko ya Kiebrania kama amri kumi.
Maswali ya kujadili juu ya wale wanaopinga Sheria za Mungu’
-          Kama amri hizo hazina haja tena sasa, kwanini wanawaongoza watu wao kutubu, nini kimefanya wajue kuwa wanapaswa kutubu tofauti na sheria?
-          Kwanini wanakemea dhambi kama vile, wizi, uzinzi,uongo nk je ni nini kilichowajulisha kuwa hizo ni dhambi? Na kama amri hizo zilishaondolewa msalabani kwanini wanaendelea kuzihubiri na huku kwa upande mwingine wanazikanusha? Au ni nini hasa wanachojaribu kukwepa katika amri ,hdi kuonyesha kutokuwa na msimamo tulivu wa kifikra juu ya amri za Mungu?
Nyongeza ya sheria za maagizo zilizoondolewa na mauti ya Yesu.
Ninaamini mpendwa msomaji wangu tuko pamoja katia mfululizo huu wa uchambuzi juu ya Sheria na Neema, ninapoelekea ukingoni kwa uchambuzi huu nimeona vema pia nikupatie mwangaza kidogo juu ya aina ile nyingine ya Sheria za Maagizo au Makafara zilizokomeshwa’
Pitia kwa utulivu sheria hizo katika maandiko mawili hapo chini, ili kuona sheria hizo ambazo Yesu alizisitisha mbali na zile amri kumi adilifu za milele.
Lawi 15:19-28
Lawi 21:1-22
-          Sheria za kafara za wanyama
-          Tohara
-          Unajisi wa damu ya hedhi na shahawa.
-          Unajisi wa wakoma.
-          Unajisi wa kushika maiti.
Kadri ya Bblia sheria hizo na nyinginezo kadhaa zilikuwa ni sheria za mpito na zilipaswa kukoma baada ya ujio wa Masihi /Yesu alifanya matukio kadhaa kama ishara ya kukomesha sheria hizo”...
-          Aligusa wakoma – Mathayo 9;18-25
-          Aliguswa na mwanamke waliyetokwa damu- Marko 5:25-34
-          Aligusa na kufufua maiti wakati wa huduma yake.
Amri kumi  za Mungu   zinadumu  milele zote / Ufunuo 14:12



TUCHUNGUZE IMANI
                                        Pr  Dominic  Mapima.
                    Somo la ‘9’ Mahubiri ya hadhara – Ukonga SDA.
MUNGU  MMOJA ’ SIKU  MOJA YA IBADA
TUMEKWISHA KUONA KUPITIA SOMO LA “KIOO CHA MSAFIRI” JUU YA MAFUNUO YA SHERIA“AMRI KUMI ZA MUNGU”.KWA NAMNA YA UPANA TUMEONA UMHUHIMU NA KAZI YA SHERIA KWA WAFUASI WA DINI KUWA SHERIA NDICHO KIOO CHA KUTUSAIDIA KUTAMBUA HALI YETU YA KIMAHUSIANO NA MUNGU, KUWAPIMA WOTE WATAKAOIBUKA NA KUDAI KUWA NI WATUMISHI PAMOJA NA KUTUSAIDIA KUTAMBUA IMANI YA KWELI NA YA UONGO. 
LAKINI IKIWA UTAKUMBUKA KATIKA UCHAMBUZI WA SHERIA “AMRI” HIZO KUMI ZA MUNGU TULIONA MOJAWAPO YA AMRI IKIGUSA JUU YA SWALA LA IBADA; fatilia rejea ya amri hiyo ya nne’
Kutoka 20:8-11 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. (9)siku sita fanyakazi, utende
                           mambo yako yote, (10) lakini siku ya Saba ni Sabato ya BWANA,
                           Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yeyote,wewe, wala mwana
                          wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala
                        mgeni aliyendani ya malango yako.(11)Maana, kwa siku sita
                        BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote
                           vilivyomo,akastarehe siku ya saba; kwahiyo BWANA akaibarikia
                        siku ya Sabato akaitakasa.
Kulingana na makusudi hayo ya sheria niliyoyainisha kwa kifupi hapo juu kama ilivyo katika somo la kioo cha masafiri, tutakubaliana kuwa ni jambo muhimu sana kuichunguza kwa kina amri hii ya ibada ili pia itusaidie kujipima na hatimaye kuona kama mwenendo wetu katika mifumo ya ibada inakubaliana na maelekezo ya mwabudiwa au vinginevyo!Hivyo nitoe wito kwako mpendwa msomaji wangu kuwa makini katika uchambuzi wa mada ili kupanua maarifa.
KWANINI MUNGU ALIWEKA MAELEKEZO JUU YA IBADA?
Ni jambo la busara kwanza kabla ya kusonga mbele na uchambuzi wa mada hii tukajiuliza swali hili muhimu kwamba kuna sababu zipi za msingi zilizofanya Mungu aweke malekezo ya ibada katika amri zake!, pasipo kuchukua muda ningependa kueleza moja kwa moja sababu mbili muhimu kama ifuatavyo:-
Sababu ya 1,
Yeye ndiye mwabudiwa hivyo ndiye hasa anayepaswa kumpa maelekezo mwanadamu vile anavyoweza kufanya katika swala zima la kumwabudu.
Isaya 45:22-23 Niangalieni mimi, mkaokolewe ,enyi ncha zote za dunia; maana
                       mimi ni Mungu; hapana mwingine.
Katika swala la ibada msikilize Mungu tu usimsikilize mwanadamu.
Mfano: binadamu hatokuokoa.
Eg; wakati wa vita ya Uganda Mhindi alisikia mlio wa bunduki na kuanza kukimbia akiwa amesahau mtoto kitandani, na alipokumbuka na kurudi kumwokoa ndipo alipojikuta anaondoka na paka aliyeenda kujificha kwenye kitanda hichohicho kwa kujifunika sambamba na mtoto.

Sababu ya 2,
Shetani naye anadai kuabudiwa na wanadamu, na daima anapinga Mungu wa kweli kuabudiwa, hivyo maelekezo juu ya namna ya kumwabudu Mungu wa kweli ni kanuni pekee ya kumwezesha mwanadamu kuwa na hakika kuwa ibada yake hiyo ni ya kumwelekea Mungu wa mbinguni.
Mathayo 4:9-10 akamwambia, haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. (10)
                         Ndipo Yesu akamwambia , Nenda zako shetani, kwamaana
                         imeandikwa, msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye
                         peke yake.
Matakwa ya shetani pia ni kuabudiwa,  hivyo ni mpinzani wa ibada kwa Mungu.
KEMEO LA YESU JUU YA IBADA ZISIZOFATA MAELEKEZO YA NENO.
Katika kuweka mkazo wa kuchunguza amri hii ya maelekezo ya ibada, ni vyema pia kuangalia jinsi Yesu mwenyewe alivyoonyesha hatari ya kupuuzia maelekezo ya Mungu juu ya ibada’.
Mathayo 7:21Si kila  mtu  aniambiaye , Bwana  Bwana  , atakayeingia  katika
                        ufalme wa mbinguni; bali yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu    
                     aliye mbinguni.
Marko 7:7-13 Nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyomaagizo ya
                     wanadamu, (12) Ninyi mwaiacha  amri ya Mungu,  na  kuyashika
                     mapokeo ya wanadamu.
Ninaamini msomaji wangu umeona jinsi Bwana Yesu mwenyewe alivyoweka bayana na kukaza umuhimu juu ya kujenga msingi wa ibada na mifumo yetu ya kidini katika maelekezo halali ya Mungu mwenyewe na si badala yeke kufata au kutii sauti za wanadamu mahali pa sauti na maelekezo ya Mungu mwanyewe.’
MAELEZO YA YESU JUU YA KANUNI YA IBADA YA KWELI.
Bwana Yesu pamoja na mambo mengine katika maelezo yake aliweka wazi kanuni ya msingi ya ibada ya kweli, swala hili pia linatilia mkazo hoja yetu ya msingi tuliyokwisha ijadili juu ya sababu ya Mungu kuweka maelekezo ya ibada, kupitia maandiko yafuatayo tunaweza kugundua kipimo halisi cha ibada ya kweli na hivyo kutupa ujasiri mkubwa wa kuanza kuchunguza kwa makini amri ile ya Mungu juu ya ibada’;
Yohana 4:24 Mungu ni roho nao wamwabudio yeye imewapasa kumwabudu
                     katika roho na kweli.
Andiko hilo maarufu la Biblia ndilo linalofunua kanuni ya ibada ya kweli, katika maelezo hayo Bwana Yesu anataja mambo makuu mawili ya msingi juu ya kanuni ya ibada ya kweli, nayo ni;
-         Kuabudu “katika roho”
-         Na “Kweli”
Kanuni hizo mbili ndizo msingi wa ibada ya kweli, kwa maana nyingine endapo muabudu atapungukiwa na mojawapo kati ya hizo basi anajiingiza mwenyewe katika karipio la Yesu juu ya wale wanaoabudu kwa kufata mapokeo ya wanadamu badala ya sauti ya Mungu.
Kwanini kuabudu katika Roho na Kweli?
“Kuabudu katika roho’ _   Kuwa na ibada halisi ya kumaanisha , inayoanzia
                                             Katika chimbuko halisi la utu wa ndani.
“Na  ‘Kweli”   Ni Ibada iliyojengwa katika mfumo au taratibu halali zilizoamriwa
                        na  Neno la Mungu / imeelekezwa na kumriwa na Mungu.
Yohana 17:17 Uwatakae kwa ile kweli, Neno lako ndiyo kweli.

JE’ NI IPI BASI IBADA ILIYOAMRIWA NA NENO LA MUNGU?
MUNGU  MMOJA ’ SIKU  MOJA YA IBADA
Ni jambo linalochanganya hisia za waumini wengi wa kidini kwa karne nyingi sasa juu ya kuelewa siku halisi moja ya ibada iliyoamriwa na Mungu, uchunguzi unaonyesha kuwa asilimia kubwa ya waumini wanaabudu lakini baila kutilia maanani swala zima la kuchunguza endapo mfumo au siku ya ibada wanayokutanika kusali ndiyo iliyoamriwa na Mungu au vinginevyo!.
Furaha ya waumini wanapokuwa katika ibada zao, kucheza na kuombewa mahitaji yao ndivyo vimekuwa vigezo vya kuhisi kukubalika kwa ibada yao na hivyo kutokuwa na muda kabisa wa kuona kama wamejengwa katika roho na kweli kadri ya maelekezo ya Yesu juu ya kanuni ya ibada halisi’.
Ikumbukwe kuwa Bwana Yesu alilaumu na kukemea hali hiyo, kama ishara ya kutokukubaliana nayo:-
Marko 7:7-13  Nao waniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyomaagizo
                      ya wanadamu, (12) Ninyi mwaiacha  amri ya Mungu,  na
                      kuyashika mapokeo ya wanadamu.
Swali’: ni siku gani hiyo ya ibada iliyojegwa katika msingi wa amri ya Mungu?
Chimbuko la siku ya Ibada ya kweli’
Siku ya ibada ya kweli katika Biblia inatajwa kuwa na chimbuko la aina ya pekee linaloonyesha umaalumu wake usiyoweza kugeuzwa na yeyote.
Huenda litakuwa ni jambo la kukushangaza kusikia kuwa siku hiyo ya ibada iliumbwa”, hii ni kumaanisha kuwa tangu Mungu alipoweka misingi ya dunia pia aliweka mfumo wa ibada, alipokuwa akiumba alikumbuka kuwatengenezea watu wake mazingira na utaratibu maalumu wa kuabudu kwa kutenga siku moja aliyoiweka maalumu katika uumbaji kwa kusudi hilo la ibada.
Hebu ona:-
Mwanzo 2:1-3 Basi mbingu na chi zikamalizika, na jeshi lake lote.(2)Na siku ya
                         saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku
                      ya saba,akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na
                      kuifanya.(3)Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa
                         kwasababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya
                      kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.
Naamini kupitia andiko hilo umeweza kuona kile nilichotangulia kusema hapo awali, kwa hali halisi Mungu alipokuwa anaumba alishabuni utaratibu mzima wa mwenendo wa dunia katika mfumo wa siku, ambapo aliumba juma moja lenye siku saba’, huwa tunaimba hata shuleni:-
“How many days in the week!!!! Kiitikio’ Seven days x 2
“Kuna  siku ngapi katika  juma!!! Kiitikio’ Siku  saba  x2
Hivyo katika mfumo huo wa juma moja la siku saba, Mungu tangu katika uumbaji wake alishatenga siku moja ambayo pamoja na mambo mengine Biblia inasema aliibariki na kuitakasa (neno takasa katika chimbuko lake la lugha asilia lilikusudia “Kutenga kwaajili ya mambo matakatifu).
Katika kuthibitisha uhalali wa mfumo huo aliouweka, Mungu mwenyewe alionyesha kielelezo kwa tendo la yeye mwenyewe kustarehe katika siku hiyo,rejea maelezo ya andiko la kitabu cha Mwanzo 2:2….akastarehe siku ya saba; akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya.
Mgawanyo wa siku katika mfumo wa uumbaji.
Kuonyesha kuwa Mungu aliweka makusudi yake katika mfumo wa uumbaji hususani juu ya swala hili la ibada ya siku hiyo ya saba(sabato), maandiko yanaonyesha kile alichokiweka  Mungu katika anga ili kuzalisha mfumo mzima wa majira katika mzunguko wa dunia.
Mwanzo 1:14 Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge
                      kati ya mchana na usiku; nayo ndiyo iwe dalili ya majira na siku na
                   miaka.
Biblia inataarifu kuwa Mungu aliweka vitu hivyo vinavyoitwa mianga ambavyo ndivyo utawala usiku na mchana na kuweka mzunguko wa siku hivyo kuzaa mfumo wa majira na hatimaye tunapata siku na miaka.Hivyo agizo la ibada linazingatia mapangilio huu wa uumbaji na hivyo basi mwanadamu anaagizwa tumia siku ile ya mwisho ya juma(Sabato)
Zaburi 19:1 Mbingu zahubiri utukufu wa Mungu,Na anga latangaza kazi ya
                  mikono yake. (Rumi 1:20)
Kutoka 20:8-11 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. (9)siku sita fanyakazi, utende
                           mambo yako yote, (10) lakini siku ya Saba ni Sabato ya BWANA,
                           Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yeyote,wewe, wala mwana
                          wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala
                        mgeni aliyendani ya malango yako.(11)Maana, kwa siku sita
                        BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote
                           vilivyomo,akastarehe siku ya saba; kwahiyo BWANA akaibarikia
                        siku ya Sabato akaitakasa.
Baada ya kuona mchanganuo huo sasa tunaweza kukubaliana na ukweli kuwa swala la ibada ni swala nyeti na rasmi sana na hivyo lingepaswa kuchukuliwa kwa umakini mkubwa kwasababu maandiko hayo ya Biblia yanaonyesha wazi kuwa swala hilo la ibada ni swala la kimfumo, tena ni mfumo ambao uliwekwa tangu kuwekwa misingi ya dunia.
JE’ SIKU HIYO YA IBADA (SABATO) NI IPI KATI YA SIKU HIZI ZA LEO? 
Bilashaka hilo ndilo swali lililo kichwani mwako ndugu msomaji wangu mpendwa!’,nami nimeona vema kupitia makala hii, niweke bayana kila kipengele ili kufunua nuru hii ya wazi inayowekewa kisogo katika kipindi hiki mfumuko wa imani na mifumo mbalimbali ya kidini.
Kanuni ya kiistoria na maandiko ya kufahamu siku ya ibada.
Biblia inafunua wazi siku hii ya kweli ya ibada katika maandiko ya kitabu cha Luka, na ili kupata picha ya moja kwa moja juu ya swali hili kupitia andiko hilo la Luka’ ni vyema kwanza tukumbushane historia:-
Jamii ya Wakristo wote tunaamini kuwa Bwana Yesu alikufa na kufufuka, kumbukumbu ya kihistoria inayokubaliwa na watu wote tangu karne na karne inaonyesha pasipo shaka kuwa Bwana Yesu aliuwawa pale msalabani siku ya “Ijumaa’ na kwa kuweka uzito wa ukweli wa hilo nikukumbushe pia kuwa katika siku hiyo baadhi ya waumini wa madhehebu ya Kikristo huadhimisha siku maalumu ianyoitwa Ijumaa kuu’ katika siku hiyo hawali nyama kama ishara ya kuhuzunikia kifo hicho cha Yesu.’
Hivyo kwakuwa jamii yote ya Waktristo inakubaliana kuwa Bwana Yesu alikufa siku ya ijumaa na kufufuka siku ya jumapili, ndivyo pia inakuwa rahisi kuelewa juu ya siku hiyo ya ibada inayotajwa na mandiko ni ipi katika mfululizo wa siku za juma kwa kulinganisha na andiko hilo  la Luka.
Luka 23:52 mtu huyu alikwenda kwa Pilato, akataka kupewa mwili wa Yesu. (53)
                 akaushusha, akauzinga sanda ya kitani,  akauweka  katika kaburi
                 lililochogwa mwambani, ambalo hajalazwa mtu bado  ndani yake.
                  (54)Na siku ile ilikuwa  siku ya maandalio, na sabato ikaanza kuingia.
                (55)Na  wale  wanawake  waliokuja  naye  toka Galilaya  walikuwa
                 walimfuata, wakaliona kaburi, na jinsi mwili wake ulivyowekwa. (56)
       Wakarudi,  wakafanya  tayari manukato  na  marhamu.  Na siku ya
       sabato walistarehe kama ilivyoamriwa.
Andiko hilo la Luka linataja kisa cha mauti ya Yesu na harakati za mazishi yake yaliyoendeshwa na Yusufu wa Al Mathaya, mtume Luka anaripoti kuwa katika siku hiyo ambapo Bwana Yesu alikufa ( Ijumaa kuu),  bwana mkubwa mmoja aitwaye Yusufu ndiye aliyeomba na kukabidhiwa jukumu zima la mazishi ya Yesu katika siku hiyo inayokubalika kihistoria kuwa ni siku ya Ijumaa.
Mtume Luka anaitaja siku hiyo ya Ijumaa ya mauti ya Yesu kwa sifa ningine kuwa ni siku ya maandalio, na ndipo hatimaye baada ya siku hiyo hufuatia siku ya sabato’
Rejea:
Luka 23:...(54)Na siku ile ilikuwa  siku ya maandalio, na sabato ikaanza kuingia.

Kumbuka Bwana Yesu alikufa msalabani saa 9 jioni, muda ambao ulikaribiana na saa kumi na mbili ambapo siku hubadilika, hata hivyo wakinamama wale walionekana wakijitokeza katika kaburi hii inamaanisha kuwa muda ulikuwa umesogea zaidi, kwa kuwa hatahivyo Biblia haitaji muda ambao Yusuph Al Mathaya aliondoka na mwili wa Yesu kuelekea kaburini, kwahiyo ni wazi kuwa masaa hayo yalikaribia muda ambao siku huisha na kuingia nyingine hasa kulingana na jukumu zito la kuushusha mwili huo na kuanza safari ya kuupeleka katika kaburi lake’ naam siku ya sabato ilianza kuingia.
Kwa uchambuzi huo ndugu msomaji wangu ni bayana kuwa siku ya saba (sabato) inayokusudiwa ni siku ya jumamosi ambayo kimsingi ndiyo hufuatia baada ya siku ya Ijumaa.’
Maandiko ya Biblia yanaweka wazi kuwa siku hiyo ya Sabato (Jumaamosi), ndiyo iliyoamriwa kupumzika, na hivyo hata wale kina mama waliokuwa wafuasi wa Yesu alirudi na kustarehe katika siku hiyo kama ilivyoamriwa.
Kidokezo:
Nenokama ilivyamriwa, lilimaanisha kwa upande mwingine kuwa hakukua na amri nyingine iliyowahi kutolewa kubatilisha hiyo ya kutunza sabato, na kwakuwa hiyo ya kutunza sabato bado ilitoka kwa Yesu pia licha kwa muda huo alikwisha kufa, basi walilazimika kundelea na utii wao kwa maelekezo hayo ya Yesu huku wakiwa wamezui shughuli ya kwenda kupaka Marhamu mwili wa Yesu hadi itakapokwisha sabato.
Rejea:
Luka 23:… (55)Na  wale  wanawake  waliokuja  naye  toka Galilaya  walikuwa
                    walimfuata, wakaliona kaburi, na jinsi mwili wake ulivyowekwa. (56)
        Wakarudi,  wakafanya  tayari manukato  na  marhamu.  Na siku ya
                 sabato walistarehe kama ilivyoamriwa
Katika sura ya 24’ ya Injili ya Luka, Biblia inaitaja siku ambayo Yesu alifufuka (jumapili) kama siku ya kwanza ya juma’
Luka 24:1-2  Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka,walikwenda
                    kaburini, wakayaleta manukato waliyoweka tayari (2) Wakalikuta
                    lile jiwe limeviringishwa mbali na kaburi.                  
Biblia inaitaja siku hiyo ya jumapili kama siku ya kwanza ya juma, kwa maana hiyo siku ya saba ya juma ni Jumamosi, swali la msingi linaweza kuibuka kuwa mbona basi majina ya siku hizi yanapingana na mfumo wa asili! Kwa kuwa endapo tukihesabu siku kwa kufatisha utamshi mfumo halisi wa siku hizo unabadilika, yaani kwa mfano: tukitafsiri mosi (jumamosi) kuwa ndiyo siku ya kwanza na pili (jumapili) ndiyo siku ya pili mfumo wa asili unabadilika.
Lakini ni vyema ieleweke kuwa majina hayo yaliyopachikwa siyo halisi na hayana uwiyano wowote na hesabu ya kiasili ya siku, hata hivyo majina haya yalipachikwa tu karne chache baadae na Wakoloni, na jambo la kushangaza ni kuwa mfumo huo tuliouzoea wa uitaji wa majina ya siku kwa kusema Jumatatu, jumanne, jumatano alhamisi ijumaa haukubalini hata na kalenda wala mfumo wa majina ya siku wa kiarabu.
Waarabu wanavyotamka majina ya siku
1
Yaumu ahad
Sunday
Jumapili
2
Yaumu ithnain
Monday
Jumatatu
3
Yaumu thalathat
Tuesday
Jumanne
4
Yaumu al’baa’
Wenesday
Jumatano
5
Yaumu l khamsy
Thursday
Alhamisi
6
Yaumu l-jamaa/ sittat
Friday
Ij umaa
7
Yaumu sabti
Saturday
Jumamosi/sabato

BWANA YESU, MITUME NA WAKRISTO WOTE WA AWALI WALITUNZA SABATO  (JUMAMOSI)   KAMWE   HAPAKUWA  NA   IBADA   NYINGINE.
Nijambo linaloshangaza kwa mtu yeyote anayetangaza kuamini Biblia, kujikita katika mfumo wa ibada nyingine yeyote tofauti na ile ya siku hii ya kweli ya saba ya juma (sabato), hilo linatokana na kile kinachoonekana kuwa watu wote wa Biblia manabii, mitume na waumini wote waliadhimisha mikutano yao mikuu ya ibada katika siku hii ya saba ya juma Sabato (jumaamosi).
Hebu tupitie ushahidi ufuatao kuthibitisha hili:-
YESU ALITUNZA SABATO/JUMAAMOSI.
Luka 4:16 Akaenda Nazareti hapo alipo lelewa, na siku ya sabato akaingia
                katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake.
Kwa andiko hilo tunaona dhahili kuwa Bwana Yesu mwenyewe aliadhimisha matendo ya ibada katika mfumo wake wa kawaida  katika siku hiyo ya saba ya juma, Sabato – Jumaamosi, na kimsingi Biblia haitaji siku nyingine ambayo Yesu alitekeleza matendo ya ibada zaidi ya siku hiyo.
Kumbuka Yesu alisema:
Mathayo 11:29 jitieni nira yangu, mjifunze kwangu, kwakuwa mimi ni mpole na
                       mnyenyekevu wa moyo…
Hivyo ni vyema kujiuliza kama ibada yako imejengwa katika imani na matendo yaliyoonekana kwa mwasisi mwenyewe wa imani yaani Bwana Yesu Kristo!, na ikiwa sivyo ni vyema kujichunguza upya na kufanya matengenezo.
Kwanini Yesu mwenyewe alikuwa akisali siku hiyo?
Biblia inatoa maelezo ya msingi yanayoonyesha sababu za msingi za Yesu mwenyewe kuhudhuria ibada katika siku hiyo ya sabato.
Ebrania 12:2 Tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza iman Yetu.
Marko 2:28 Basi mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato pia
Hivyo kwa kifupi alipaswa  kunyesha  kilelezo  kama  mwasisi  wa ibada ya kweli, na hivyo kuacha mfano wa namna ibada ya kweli inavyopaswa kuwa.
MITUME WALITUNZA SABATO/JUMAAMOSI.
Baada ya Yesu kupaa mbinguni aliwaacha mitume wake ambao kimsingi ndiyo waliokuwa wakiendeleza msingi wa imani aliyoicha Bwana na mwalimu wao Yesu Kristo, hivyo kadri ya maandiko mitume hawa wanatajwa kuwa ni kioo cha msingi wa kweli wa imani. Bwana Yesu alitamka maneno ya msingi sana yanayotia muhuri maelezo haya:-
Yohana    awapokeaye ninyi, anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea
                   yeye aliyenituma.
Kwakuwa mitume hao walitarajiwa kufanya kile Yesu alichokianzisha, basi  Bwana Yesu mwenyewe katika andiko hilo anawatambulisha mitume hao kuwa wangestahili kupokelewa kwakuwa kuwapokea au kuwaamini mitume hao kwa kile watakachofundisha na kutenda kadri ya mfano wa Bwana na mwalimu Yesu Kristo il kuwa sawa na kusikiliza Bwana Yesu mwenyewe.
Ndipo kwa msingi huu mtume Paulo aliwahi kutamka.
1Wakoritho 11:1 Mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo.
Tamko hili la mtume Paulo linaonekana kugusa vizuri nyanja hii ya ibada kwa kile tunachosoma kadri ya maandiko kuwa mtume huyo Paulo mwenyewe aliendeleza kanuni ileile ya ibada ya Yesu kwa kuhudhuria ibada katika masinagogi na kuendesha mijadala ya kidini siku ya Sabato.
Matendo 17:1 Waakisha   kupita   kati   ya   Ampifoli , na   Apolonia  wakafika
                         Thesalonike, ambapo palikuwa na Sinagogi la Wayahudi. (2) Na
                      Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo,
                      akahojiana nao kwa maneno ya maandiko Sabato tatu.
Hivyo mtume Paulo anasimama kama shuhuda wa kudumu kwa msingi wa ibada hiyo ya kweli ya siku ya Sabato ya Bwana (Jumamosi), naye anafanya kilekile alichokifanya Yesu, yaani kuhudhuria ibada za masinagogi kama ilivyokuwa desturi yake ndiyo uliokuwa mfumo wake wa siku zote katika misha ya ibada.
Pamoja na ushahidi huo wenye nguvu, bado Biblia inatoa ushahidi wa kutosha tu juu ya kudumu kwa maadhimisho ya ibada kuu za mikusanyiko katika siku hii ya saba ya juma (Sabato)katika vipindi mbalimbali vya mwendo wa safari ya imani wa mitume na wajenzi wa kanisa la awali, tuone ushahidi wa maandiko mengine juu ya kudumu kwa utunzaji wa siku hii ya kweli ya ibada Sabato katika ulimwengu wa kale wa mitume na wafuasi wa Bwana Yesu mara baada ya kupaa kwake mbinguni.
Matendo 13:13-15.. lakini   wao  wakang’oa  nanga   wakasafiri  kutoka  Pafo,
                              wakafika Perge katika Pamfilia. Yohana akawaacha akarejea
                              Yerusalemu. (14) Lakini wao  wakatoka  Perge,  mji  mmoja wa
                            Pisidia, wakaingia  katika  Sinagogi siku ya Sabato, wakaketi.
                               (15) Kisha, baada ya kusomwa Torati na chuo  cha  manabii ,
                            wakuu wa sinagogi wakatuma  mtu   kwao, na   kuwaambia,
                               Ndugu,kama mkiwa na neno la kuwafaa watu hawa,lisemeni.
Hapa tena tunaona mitume wakiadhimisha ibada katika siku hiyo ya Sabato, na kikubwa tunaona watu waliokuwa katika Sinagogi walionyesha kutambua uwepo wao na kuwa karibisha kutoa neno katika siku hiyo ya ibada ya Kibiblia, kwajumla mandiko ya Biblia yako wazi sana katika hili nap engine niseme kuwa fundisho la siku ya ibada ndilo fundisho la wazi sana na lenye ushahidi wa kutosha katika Bilblia, fanya uamuzi wa kufata Biblia.
Ushahidi mwingine / Kanisa lilitambua ibada ya siku ya Sabato pakee.
Uchambuzi wetu utaishia katika kisa hiki cha safari ya watumishi wa Mungu wa awali katika safari yao ya kuhimarisha makanisa, ambapo tunaona bado wakitoa picha ya kudumu kwa maadhimisho ya ibada ya kweli katika siku hii ya Sabato:-
Matendo 16:4,5,13,16,17
Basi walikuwa wakipita katika miji ile, wakawapa zile amri zilizoamriwa na mitume na wazee waliyoko Yerusalemu, ili wazishike. (5) Makanisa yakatiwa nguvu kwatika ile imani, hesabu yao ikaongezeka kilasiku.
(13)Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani yakuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale.
(16) Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, kijakazi kimoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua. (17)akamfuata Paulo na sisi akapiga kelele akisema, watu hawa ni watumishi wa Mungu aliye juu, wenye kuwahubiria njia ya wokovu.
Andiko hilo kwa ujumla wake, lnaonesha hali halisi na picha ya mwenendo wa kanisa la mitume namna lilivyodumu kutunza siku ya kweli ya ibada ya Sabato, Paulo na wenzake wanaonekana kuchukua jukumu la kusafiri ili kuhubiri Injili na kuhimarisha makanisa nyuma ya agizo la baraza la wazee na mitume lililoketi katika mji wa Yerusalemu na kutoa maelekezo mbalimbali ambayo yangesaidia kuleta kuhimara na ukuaji wa kanisa.
Katika ziara inayoelezwa katika mafungu hayo, Paulo na wenzake wanaonekana kuendelea kudumu kuadhimisha tendo la ibada katika siku hii ya kweli ya sabato, (Matendo 16:13)Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani yakuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale. 
Banafsi huwa ninapatwa na uzuni kubwa sana ninaposoma maandika haya na kulinganisha na hali tuliyonayo sasa ya mipasuko ya kidini iliyozaa siku mbalimbli za maadhimisho ya ibada zisizo za kimaandiko.
Ni vyema ieleweke kuwa kama Yesu angefanya au kuamuru mabadiliko yeyote juu ua siku ya ibada, basi watu wa kwanza ambao wangetekeleza ni mitume wake ambao kimsingi waliishi muda kadhaa mara baada ya kifo na ufufuko wa Yesu.
TUNAWEZAJE KUJUA KUWA SABATO HII’ JUMAMOSI NDIYO HALISI?
Mhubiri 3:11  kilakitu amekifanya kizuri kwa wakati wake’ tena ameiweka hiyo
                        milele ndani ya miyoyo yao; ila kwajinsi mwanadamu asivyoweza
                     kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya tangu mwanzo hata
                     mwisho.
               14   Najua yakwamba kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele,
                     haiwezekazi kuzidisha kitu, wala kuipunguza kitu, nayo Mungu
                     ameifanya ili watu wamche
kitabu hicho cha mhubiri kinatoa majibu ya swali hilo muhimu kwa kuonyesha njia na kusudi la Mungu mwenyewe kulinda yale aliyoyaweka yeye mwenyewe ili yasiharibiwe na yeyote.
Andiko hilo linaonyesha kuwa Mungu hutumia miyoyo ya wanadamu wenyewe kuhifadhi maarifa ya uzuri wa kazi yake, na kwa kadri ya historia tunaweza kuona jinsi mwanadamu mwenyewe alivyoshiriki kulinda mifumo muhimu ya uumbaji wa Mungu hususani mzunguko wa siku:-
Historia inaonyesha:
Tangu karne nyingi watu walitunza mzunguko wa siku bila kupoteza mwelekeo kwa kutumia SOLAR CALENDER – yaani kalenda ya asili ya mfumo wa mzunguko wa dunia wa uumbaji, unaohusisha Jua, Planets, and other bodies – na viumbwa anga vingine vinavyofanya mzunguko wa dunia.
Kwajumla katika katika mfumo huu wa asili mwenendo wa jua ndiyo uliotoa mwelekeo wa hesabu ya mzunguko wa masaa, hivyo kupata siku miaka na miezi.
§  Mwaka 350 kk, ilitumika njia ya asili ya kufata kivuli cha binadamu kinavyosogea kwa kufuata mwanga wajua.(watu walitunza mzunguko wa masaa na siku kwa njia hiyo).
§  Karne ya 4’ mjapani Lntern Clock aligundua saa ya kutumia mashine iliyoitwa Horogum kabla ya kuitwa Clock
§  Ndipo karne ya 8’ saa kongwe ilibuniwa na kuanza kutumiwa ambayo imehifadhiwa katika jumba kongwe kule Misri.
§   Na baadae ilifatia saa nyingine ya mjapani Enly De Vick, ambayo ilitumika katika jengo la mahakama kule Ufaransa ikiwa na Urefu wa futi 37’ na kilo 237’
§  Wataalamu wengine waliongezeka kama vile: mzungu George Graham, Mholanzi Christian Hygens na baadae kugundulika teknolojia ya kutengeneza mizani na mwanafizikia Robelt Hook.
Kutokana na teknolijia ile ya asili na ile ya saa kusaidia kutunza hali ya mzunguko wa siku ndiyo maana historia pia imefanikiwa kutunza kumbukumbu ya tarehe ama miaka ya matukio muhimu duniani.
Wanahistoria wanagawa miaka katika makundi mbalimbali ikiwa ni matokeo ya uwezekano wa kunza rekodi ya mzunguko wa dunia;-
Mgawanyo wa siku na miaka kihistoria:-
Day            duration of twenty four hours / Kipindi cha masaa ishirini na nne.
Week          duration of seven days/ kipindi cha siku saba
Year           duration of twelve months/ kipindi cha miezi kumi na mbili.
Decade     duration of ten years/kipindi cha miaka kumi.
Century     duration of one hundred years/kipindi cha miaka miamoja.
Millenniumduration of one thousand years/ kipindi cha miaka elfu moja.
Age             a period based on man’s economic activities and the types of tools
Kwa mtu mwenye kutafakari atakubaliana na ukweli kuwa tendo la kuwezekana kutunzwa na kumbukumbu za matukio sahihii kwa miaka na karne nyingi za nyuma ni ushahidi tosha kuwa hakuna makosa yeyote juu ya maadhimisho yanayofanywa na waumini wa dunia nzima ya kuadhimisha mikutaniko ya ibada katika siku hii ya kweli ya sabato kadri ya mfumo wao wa kijografia wa mzunguko wa siku.









 

No comments:

Post a Comment